Home
Page
Contact
Us
Make a Payment,
Methods of
Payment, Refund and Exchange Policies
Rosaries
subpages:
How to Pray the
Rosary
subpages:
Pictures
Main Page
subpages:
Curriculum
subpages:
Website
Terms of Use
License
Agreement
Sitemap
The Work of God's Children
|
Kiswahili
Rosary
Prayers
This language is also
known as Swahili and Kisuaheli.
This language is spoken by 30,000,000 people in
Zanzibar, Burundi, Kenya, Mayotte, Mozambique, Oman, Rwanda,
Somalia,
South Africa, and
Uganda.
See also The
Work
of God's Children page for the illustrated version of
prayers
in this language.
Rozari Takatifu Ya Kibiblia Ya Bikira Maria Mtakatifu / The Holy Rosary
Ishara Ya
Msalaba / The Sign of the Cross / Signum Crucis
Kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina!
Nakuungamia / Apostles'
Creed / Credo
Nakuungamia kwa Mungu baba Mwenyezi,
Muumba wa Mbingu na nchi na Kwa Yesu Kristo mwanaye wa pekee.
Aliyezaliwa na bikira Maria kwa uwezo wa roho mtakatifu. Akateswa kwa
mamlaka ya ponsio pilato,Akasulubiwa, akafa, akazikwa na kushukia
kuzimu. Siku ya tatu akafufuka katika wafu, akapaa mbinguni, Amekaa
kuume kwa baba na atakuja tena kwa utukufu kuwahukumu wazima na wafu.
Nasadiki kwa roho mtakatifu, Kanisa takatifu Katoliki ushirika wa
watakatifu, maondoleo ya dhambi, ufufuko wa miili na uzima wa milele
AMEN.
Baba
Yetu / Our
Father / Pater Noster
Baba yetu uliye
mbinguni, jina lako litukuzwe.
Ufalme wako ufike. Utakalo lifanyike duniani kama mbinguni.
Utupe leo mkate wetu wa kila siku.
Utusamehe makosa yetu,
kama tunavyowasamehe na sisi waliotukosea.
Usitutie katika kishawishi,
lakini utuopoe maovuni.
Amina.
Another version of
Baba
Yetu
/
Our Father / Pater Noster
Baba yetu uliye mbinguni,
Jina lako litukuzwe,
Ufalme wako
uje,
Mapenzi yako yatimizwe,
hapa duniani kama huko
mbinguni.
Utupe leo riziki yetu.
Utusamehe deni zetu,
kama
sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu.
Na usitutie
majaribuni,
lakini utuokoe na yule mwovu. Amina.
Doxology
Kwa kuwa ufalme ni
wako, na nguvu, na utukufu, hata milele.
Salamu Maria /
Hail Mary / Ave Maria
Salamu, Maria, umejaa neema, Bwana yu nawe,
umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu,
mzao wa tumbo lako amebarikiwa.
Maria mtakatifu, Mama wa Mungu,
utuombee sisi wakosefu, sasa na saa ya kufa kwetu.
Amina.
Atukuzwe Baba /
Glory Be to the Father / Gloria Patri
Atukuzwe Baba, na Mwana na Roho Mtakatifu.
Kama mwanzo, na sasa, na siku zote, na milele.
Amina.
Kubarikiwe siku zote
Kubarikiwe siku zote kutungwa mimba bila dhambi ya asili kwa Maria
Mtakatifu, Mama wa Mungu na Mama yetu.
Ee Yesu wangu / Oh, My Jesus
Ee Yesu wangu, utusamee dhambi zetu, utukinge na moto wa milele, ongoza
roho zote Mbinguni hasa za wale wanao hitaji zaidi Huruma yako.
SALAM, MALKIA!
/ Hail, Holy Queen / Salve Regina
Salam,
Malkia! Mama mwenye huruma uzima tulizo matumaini yetu. Salam!
Tunakusihi ugenini sisi wana wa Eva. Tunakulilia tukilalamika na
kuhuzunika huku bondeni kwenye machozi. Haya basi mwombezi wetu
utuangalie kwa macho yako ya huruma, Na mwisho wa ugeni huu utuonyeshe
Yesu mzao mbarikiwa wa tumbo lako. Ee mpole, Ee mwema, Ee mpendelevu
Bikira Maria.
NAMNA YA KUISALI
* Baada ya ishara ya msalaba,
tunasali Atukuzwe Baba na zile sala pili za
utangulizi, halafu tunalitangaza fumbo; inafuatiwa na Baba yetu
(1),Salamu Maria (10) halafu Atukuzwe Baba… na zile sala
pili za utangulizi.
Halafu tunatangaza fumbo linalofuata na kuendelea kama
ilivyoelezwa hapo juu.
* kwa namna ya pekee wakati
wa kusali “Baba yetu” na “Salamu Maria” (10) fanya akili (na moyo!)
“kukimbilia” kutafakari juu ya fumbo lililotangazwa.
MAFUMBO YA UUMBAJI
( kwa Jumatatu
) :
- YHWH: Mungu Baba kwa
njia
ya
Neno (ΛΟΓΟΣ - VERBUM),
[“Awe!”], aumba mbingu na dunia na Roho
Mtakatifu
ambaye tayari aliutangulia uumbaji kwa hekima yake alikuwa akielea juu
ya maji yaliyo kuwa yameufunika uso wote wa nchi akivibariki viumbe.
- Mungu amuumba mtu, mwanamme
na mwanamke, wote aliwaumba kwa mfano na sura yake.
- Mungu amwahidia mwanmke baada ya
dhambi ya asili kuwa kwa njia ya uzao wake, Masiha ataponda kichwa cha
nyoka – adui wa mwanadamu.
- Melkisedeki kuhani mkuu atoa mkate na divai kama
sadaka ya shukrani kwa ushindi wa babu mtakatifu Abrahamo (Mwa.
14, 18-20).
- Abrahamo aupokea ugeni, atambua na “kumkaribisha”
Bwana, Utatu Mtakatifu karibu na mialoni ya Mamre (Mwa. 18, 1-15).
- Mungu amweka huru Isaka toka mauti kulingana na ahadi
yake (“uzao
wako utakuwa mwingi kuliko nyota za mbinguni na kuliko mchanga ulioko
pwani ya bahari na kuimiliki miji ya adui zako” – (Mwa. 22, 17) na
kuimarisha Agano lake na Abrahamo (“na katika uzao wako mataifa
yote ya dunia watajibarikia” (Mwa. 22, 18).
MAFUMBO YA NGUVU
ZA MUNGU
( kwa Jumane
) :
- MUNGU, katika nafsi yake, awaokoa watu wake toka
utumwani Misri na kuizindua Pasaka ya kwanza ya “umilele” (Kut.
12,
1-15).
- MUSA
– mfano wa KRISTO - kwa Bakora aigawanya bahari ya Sham kwa ajili ya
njia na uzima wa taifa teule na kuwaangamiza maadui wa Israeli
kama
isemavyo zaburi ya pili (Zab. 2, 8-9) ya mfalme masiha “uniombe,
nami
nitakupa
mataifa kuwa urithi wako, na miisho ya dunia kuwa milki
yako. Utawaponda kwa fimbo ya chuma, na kuwavunja kama chombo
cha mfinyanzi.” na kama kisemavyo kitabu cha ufunuo wa
Yohana (Ufu. 12, 5) “naye atamzaa mtoto wa kiume atakaye
yatawala mataifa yote kwa fimbo ya chuma na mtoto alichukuliwa
mara moja mbele ya Mungu na mbele ya kiti chake cha enzi”.
- NGUVU
YA MUNGU, katika namna ya wingu ikatulia juu ya sanduku la agano Ambalo
lilikuwa limewekwa katikati ya kambi ya wana wa Israeli ambalo katikati
Yake kuna tabernakulo takatifu ambamo ndani yake Mungu ana kaa na
ambamo taifa teule litapewa ishara tatu zilizokielezo cha
Ekaristia Takatifu na Tabernakulo ya Ekaristia Takatifu: Vibao vya
Sheria, yaani Neno lake (Verbum), “lililoandikwa kwa kidole cha
Mungu” (hivyo kuja kwake moja kwa moja kama
Mwana); Bakora ya Musa ni ishara nguvu aliyopewa na Mungu
ambayo kwayo Musa aliigawanya ya Sham; Manna iliyoshuka toka
mbinguni na ambayo huwashibisha wana wa Israeli huko jangwani.
- MUNGU
amchagua Daudi na kumpaka mafuta kama Mfalme na Nabii juu ya watu wake
Israeli na kuahidi Ufalme Milele kwa mwanae (katika uzao wake).
- JUDITA (Jd. 8-16),
anayekata kichwa cha mfalme, adui wa wana wateule akiwaweka huru toka
utumwani ni mfano wa MARIA aliyevaa jua na mwezi chini ya miguu yake na
taji la nyota kumi na mbili ambayo huseta kichwa cha mfalme wa giza,
“nyoka wa kale”, na kuwaweka huru wateule wa Kristo toka utumwa wa yule
mwovu.
- NGUVU YA ROHO MTAKATIFU inajionyeshe pia Katika
ushahidi wa mzee Eleazaro (2 Mak. 6, 18-31), katika
watakatifu ndugu wa Makabayo na Mama yao Mtakatifu (2 Mak. 7, 1-41),
kwa
kutokukubali
kuiasi Sheria ya Mungu.
MAFUMBO YA FURAHA / The Joyful
Mysteries
( kwa Jumatano ) :
- Malaika mkuu Gabrieli ampasha habari Bikira Maria, na
kwa “NDIYO” Yake, NAFSI YA PILI YA UTATU MTAKATIFU
INAJIMWILISHA KATIKA TUMBO LAKE.
- Maria Mtakatifu amtembelea Mtakatifu Elizabeti.
- YESU ANAZALIEWA BETLEHEM.
- Yesu anatolewa Hekaluni.
- Yesu anakutwa Hekaluni.
MAFUMBO YA MWANGA / The Luminous
Mysteries
( kwa Alhamisi ) :
- Yesu anabatizwa katika mto Jordan na Yohana
Mbatizaji. –
(Yesu anajipeleka kwa Yohana Mbatizaji ili aweze kubatizwa naye. Yeye
habatizwi kwa ajili ya toba bali anapenda “kujishusha” zaidi na
kujifanya mdhambi (ila bila dhambi) kati ya wadhambi. Mara baada ya
kuingia majini mbingu zinafunguka, Roho Mtakatifu katika umbo la njiwa
anatua juu yake na sauti ya Baba inatangaza toka juu mbinguni “Huyu ni
Mwanangu mpendwa wangu niliyenipendezwa naye” - Mt. 3, 17).
- Yesu anafanya ishara ya kwanza katika maisha yake
hadharani katika harusi ya Kana. - (Yesu
alikuwa amealikwa pamoja na wanafunzi wake katika harusi ya Kana ya
Galilaya. Wakiwa wameishiwa divai Yesu analetewa ombi na mama yake,
anabadili maji kuwa divai. Injili inayoeleza tukio hilo inataarifu
maneno ya mwisho ya mama Maria akituonya na kutualika daima kwamba
«LOLOTE ATAKALOWAAMBIA, FANYENI !» - Yn. 2, 5).
- Yesu atangaza ujio wa ufalme wa Mungu. -(Yesu
anatangaza kuwa ufalme wa Mbinguni u karibu na kwamba uko tayari kati
yetu na kuthibitisha kuwa wataingia humo wale tu walioisafisha mioyo
yao na kujinyenyekesha hata kujifanya «wadogo» kama mtoto).
- Yesu anabadilika sura katika utukufu wa Mungu juu ya
mlima Tabor pamoja na Musa na Elia. - (Yesu
anapanda mlima Tabor akiwa pamoja na Pietro, Yakobo na Yohana ili
kusali. Mara kwa ghafla anabadilika sura katika utukufu wake wa kimungu
anangara kuliko jua, karibu naye wanatokea Musa na Elia wakijadiliana
kuhusu utume wake wa kimasiha kwa ajili ya wokovu, kwao yampasa
aikabili Yerusalemu. Baba anatualika na anamtolea tena ushuhuda “Huyu
ni Mwanangu mpendwa wangu ninayependezwa naye: MSIKILIZENI
YEYE” - Lk. 9, 35).
- Yesu akiwa anaadhimisha Pasaka ya Kiebrania pamoja na
Mitume wake katika ukumbi wa mlo wa jioni aliweka Ekaristia Takatifu. -
(Juu
ya mlima Sion, katika ukumbi wa Chakula cha Jioni, Yesu, akiwa
anaadhimisha Pasaka ya Kiebrania pa moja na Mitume wake baada ya kuwa
amewaosha miguu aliwapa mkate na divai akithibitisha ni mwili wake na
damu yake vilivyotolewa kwa ajili ya wokovu wa watu wote. Ni adhimisho
la Ekaristia Takatifu).
MAFUMBO YA UCHUNGU / The Sorrowful
Mysteries
( kwa Ijumaa ) :
- Yesu asali katika bustani ya Getsemani.
- Yesu anapigwa mijeredi.
- Yesu anavikwa taji la miiba na anahukumiwa kifo bila
hatia.
- Yesu anapanda Calvari akibeba Msalaba.
- YESU AFA MSALABANI.
MAFUMBO YA UKIMYA
WA MUNGU
UKIMYA UNAOFANYA KAZI YA
MAPENDO NA YA HURUMA
( kwa Jumamosi ) :
- KRISTO,
kati ya siku ya kufa na siku ya kufufuka kwake, siku ya “ukimya wa
kimungu” aziweka huru roho za wenye haki na kuwaandalia nafasi mbinguni
wao pamoja na wenye haki wengine watakao fuata.
- MARIA,
kwa Upendo ya Kimama na Mama wa Kanisa zima, kwa licha ya Uchungu wa
Kalvari, licha ya “upanga” uliompenya Moyo wake pale Kalvari anapata
faraja, anatiwa moyo na kukaa siyo tu na Yohana bali hata Pietro na
Mitume wengine wakiwa na uchungu, kuchanganyikiwa na usumbufu wa
“kashfa” ya Msalaba.
- Huruma ya BABA kwa wanadamu
haikatizwi na dhambi ya kumwaga damu na kumwua Mwanae-masiha Yesu
Kristo, bali anaipokea kama sadaka jumla ya ukombozi wa wanadamu ambao
Mungu aliwapenda, akawaumba kwa sura na mfano wake na kwa ajili ya
wokovu wao akamtuma Mwanae wa pekee.
- MBEGU
iliyoanguka chini kwenye udongo ikafa, maisha ya Kristo yaliyo tolewa
sadaka na damu yake iliyo mwagika Kalvari vinachipusha leo hii toka
katika ukimya wa kimungu maisha mapya na yasiyaharibika kwa wale
wanaoupokea kulingana na mapenzi ya moyo wa Kristo.
- ROHO
MTAKATIFU, katika kimya kikuu cha Jumamosi anaiandaa na kuifinyanga
mioyo na akili za wampendao Mungu ili kulipokea tangazo la Ufufuko
lisiloweza kuaminika kibinadamu kwa wale wampendao Mungu, kulipokea
lisiloaminika (kibinadamu). Kwa tangazo la ufufuko, maana yeye, Yesu
Kristo, “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa
Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu: vyote
vilifanyika kwa huyo, wala pasipo yeye hakikufanyika chochote
kilichofanyika. Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa
nuru ya watu…Yeye ni Mwanzo na Mwisho, mwezayote …Yeye ni Mwana kondoo
asiye na hatia milele yote yuko juu ya altare ya mbinguni na yeye tu
mwenye kustahili kuchukua kitabu, kuvunja mihuri yake na kukifungua na
kumkabidhi Baba kwa utukufu wa milele wa Mungu, wa malaika zake na
watakatifu wake”.
MAFUMBO YA UTUKUFU / The Glorious
Mysteries
( kwa Jumapili ) :
- YESU ANAFUFUKA.
- YESU ANAPAA MBINGUNI.
- ROHO MTAKATIFU ANAWASHUKIA MITUME WAKIWA
PAMOJA NA BIKIRA MARIA.
- Bikira Maria APALIZWA mbinguni.
- Bikira Maria AVIKWA TAJI Mbinguni Malkia wa Mbingu na
Nchi.
Mtakatifu
Mikaeli / Prayer to Saint Michael, the Archangel
Mtakatifu
Mikaeli, Malaika Mkuu,
Utulinde
katika
vita;
Uwe
kinga yetu katika maovu na mitego ya Shetani.
Tunakuomba
kwa
unyenyekevu
Ee
Mungu mweke Shetani chini ya mamlaka yako
Nawe
Mkuu wa Majeshi ya Mbinguni,
Kwa
nguvu ya Mungu,
Mtupe
Shetani motoni
Na
Pepo wabaya wote ambao;
Wanazungukazunguka
duniani,
Wakitafuta
kuangamiza
roho
za watu. Amina.
Another version of
Mtakatifu
Mikaeli Malaika Mkuu / Prayer to
Saint Michael, the Archangel
Mtakatifu
Mikaeli
Malaika
Mkuu, utulinde katika vita, uwe kinga yetu katika
maovu na maoteo ya shetani, Mungu amtiishe tunaomba sana, nawe Mkuu
wa Majeshi ya Mbinguni, kwa nguvu ya Mungu, uwaangushe motoni shetani
na pepo wabaya wengine wote, wanaozunguka duniani,ili kuzipoteza roho
za watu. Amina.
Usiku wa sifa /
Silent Night
Usiku wa sifa
Wa raha na nuru
Alipozaliwa Mwana
Mtakatifu na mwema
Mwana ndiye Mungu
Mwana ndiye Mungu
"God
is
Love"
in Kiswahili is " Mungu ni Upendo. "
|